Wushu"ya Waislamu wa China na jinsi ilivyowasaidia
kupambana na dhulma dhidi yao.
"WAISLAMU hodari kumi tu waliolinda nchi". Huo ni mmoja ya misemo
mashuhuri katika enzi za Yuam nchini China ikiisifu juhudi ya Waislamu
kutokana na uhodari wao wa juu katika "wushu" (sanaa ya mapigano).
MUSSA ALLY anaielezea zaidi "Wushu"ya Waislamu wa China na jinsi
ilivyowasaidia kupambana na dhulma dhidi yao.
HIVI leo huwezi ukaizungumzia historia ndefu ya sanaa ya mapigano ya
Uchina na ikawa kamili bila kutaja mchango wa Waislamu katika kuiboresha
fahari ya taifa hilo (
martial art), ambayo kwa sasa imeshatoka nje
ya mipaka ya nchi hiyo ya Asia na kuendea kote duniani.
Ujasiri wa kutenda, nidhamu iliyokomaa (si nidhamu ya woga kama walivyo
baadhi ya Waislamu wa Tanzania). Afya njema, utoaji wa hoja zenye mashiko,
umoja, hekma, na nguvu inapohitajika ni miongoni mwa sifa za msingi za
Waislamu wa China zinazoinawirisha sanaa ya kisasa ya mapigano ya nchi
hiyo.
Mapambano ya kutumia mikono kwa kubadilishana makonde sura kwa sura,
mtu na mtu au mtu na watu ni moja ya aina za wushuya Waislamu.
Kutumia ala nzito na nyepesi, fupi na ndefu, kali na butu ni sehemu
nyingine ya Wushu ambayo Waislamu wa China wanajivunia kuwa nayo.
Tukirejea katika ngumi (makonde) moja ya aina mashuhuri za ngumi ambazo
Waislamu wanatumia toka katika utajiri wao mkubwa wa "Wushu" ni makonde
ya "cha" yaliyoanzishwa katika zama za Ming na kuimarika vyema wakati wa
Qing.
Mwanzilishi wa makonde hayo ni kijana mbichi aliyeitawala Chamir, aliyetokea
China Magharibi.
Kwa mujibu wa historia ya Waislamu China kijana huyo mwenye moyo thabiti
wa kimapindizi na nia ya kujifunza, alikuwa katika wito wa mfalme wa kuwatimua
wavamizi wa Kijapani katikati ya enzi za Ming ambapo alijivuta hadi kijijini
Zhangyin Zhuang wilayani Guan mkoani Shandong alipopata maradhi ya homa
ya matumbo.
Hapo alipokelewa na Waislamu waliomuuguza vyema hadi kupona kwake. Ni
wakati huo kijana Chamir alipowafunza Waislamu hao staili moja ya makonde
kama shukrani ya kumkirimu.
Kwa heshma na kumbukumbu yake, Waislamu wa Zhangyin Zhuang wakayaita
makonde hayo jina la Chamir kwa kifupi "Cha". Na tangu hapo aina hiyo ikavuka
mipaka ya Guan na kuendea katika maeneo mengine ya nchi.
Historia inatufuhamisha kuwa kwa ujumla Wushu ya Waislamu wa China ina
tabia ya Wushu ya kabila la Wahan na tabia nyingine ya kabila la Wahai
ambayo ni miongoni mwa makabila 56 yanayofuata Uislamu ipasavyo nchini
China, yakiwa na jumla ya Waumini wasiopungua milioni 14 na misikiti isiyopungua
30,000 mikoani kote.
Katika maandiko yake kuhusiana na Uislamu nchini China, msomi mashuhuri
wa Kiislamu nchini humo Bw. Feng Jinyilan katika kile alichokiita: "Marejeo
teule juu ya Uislamu Uchina" pamoja na Bw. Li Xinghua wakieleza historia
ya jamii hiyo, wanaonisha wazi kwamba nyakati za mwisho za zama za Ming,
sanaa ya mapigano (martial Art) ilikuwa mashuhuri na kutandawaa nchi nzima.
Mnamo mwaka 1642Bw. Li Zicheng kiongozi wa Mapinduzi ya Wakulima alizunguka
mji wa Chengzhou.
Miongoni mwa wapiganaji alio watumaini mno, ni wale mastadi wa Wushu
wa Kiislamu wasiopungua 300 waliokuwa chini ya imamu katika kambi maalumu.
Pia alikuwapo jemedari wa Kiislamu aliyeitwa Ma. Shaouying aliyeongoza
kikosi cha Waislamu kilichojiunga na mapinduzi ya mwishoni mwa enzi yautawala
wa Ming uliong’olewa mamlakani na madarakani mapema mwaka 1644. Huo ni
ushahidi wa wazi wakuonyesha mchango wa Wushu ya Kiislamu katika kuleta
mageuzi nchini China..
Historia inatufahamisha kwamba mnamo mwaka 1616 hadi 1911 (Enzi ya Qing)
dhulma, unyanyasaji uliopea (umwembechai) toka kwa watawala wenye mamlaka
na madaraka katika jamii iliogubika jamii ya Waislamu.
Hivyo basi Waislamu hawakuvumilia "umwembechai" huo dhidi yao, wakaanzisha
mapambano makubwa ya mfululizo dhidi ya madhalimu –"wanaowamwembechai..
"Waislamu walitambua kwamba wakitaka kulinda dini yao, iliwabidi kuwa
na afya njema, kwa hiyo hulka za ujasiri, umoja na kutoogopa watu wenye
mabavu zikalelewa na kuimarishwa. Katika misikiti ya kila pahala zilitengwa
nyanja za kufanyia mazoezi ya Wushu kila saa za asubuhi, jioni na baada
ya sala, watu wote (waumini wote) walijikusanya pamoja kufanya mazoezi
ya kuinua ustadi wa Wushu (sanaa ya mapigano). Katika hali hii ya mazingira
ya kijamii, wushu ya Waislamu iliendelea kwa upesi na wakatokea wanafunzi
hodari wa Wushu kizazi kwa kizazi", rejea Feng Tinyuan kwenye Uislamu katika
China, wushu ya Waislamu Uk. 71-72. Foreing language press Baiwanzhuang
– Beijing.
Tarehe inaonyesha wazi kwamba mwaka 1911 hadi 1949 (zama za Jamuhuri
ya Uchina) kabila la Wahui (ambalo ni moja ya makabila ya Waislamu) kulikuwa
na mabingwa wengi mno wa Wushu ukimuacha bingwa mashuhuri Bw. Liu Baonii.
Miongoni mwao ni Chan Zhengfang, muumini mzuri wa Kiislamu kijijini
Zhanyying Zhuang, wilayani Guan huko Shandong.
Bwana huyu alihamia Honan mbeleni. Uhodari wake wa sanaa ya mapigano
uliwaacha wengi vinywa wazi.
Matunda yake ni pamoja na mabingwa mashuhuri hivi leo nchini humo na
duniani kiujumla kama kina Zhanga Xitai, He Zhengquan, Ma Zhenbag na wengineo
wengi walioendea hasa katika mikoa ya Shanzi, Hebei, Shandong, Honan, Shaanxi,
Jiangsu, Shanghai na hata Hubei.
Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni za kile kinachojulikana kama
"China mpya", asili ya wanawushu wa Kiislamu wa kabila la Hui, imepata
maendeleo maradufu.
Mnamo katikati ya karne hii, waumini wa Kiislamu wa Shandong na Hebei
wameasisi taasisi muhimu ya kuchunguza kwa undani zaidi sana ya mapigano
ya Kiislamu toka kabila la Wahui.
Chama cha sanaa ya mapigano ya Kiislamu katika misikiti kikaasisiwa
kuendeza fani hiyo kwa ummah.
Wakawataka mastadi wa Wushu ya Kiislamu kuzama chini mno katika sanaa
hiyo azizi hivyo kurejesha utaalamu wa Wushu wa kale ili usipotee.
Hivi sasa wanataaluma hiyo wenye ubingwa wa hali ya juu sana katika
umma wa Kiislamu Uchina, wananza kupokea kwa wingi wanashule wa rika zote
(wazee, watoto kwa vijana, wake, kwa waume) kuwafunza wushu; na mkazo mkubwa
umewekwa kwa kizazi kipya, na matunda yake yanaendelea kuonekana.
Kwa mujibu wa mtafiti mashuhuri wa Kiislamu, Feng Jinyuan, wushu ya
Kiislamu ya kabila la Wahui inatabia zake mahsusi, ameainisha baadhi yake
kama ifuatavyo:-
Waislamu wa Kihui wanahistoria ndefu ya uchezaji wa wushu. Kila kizazi
kilikuza na kinaendelea kutoa mastadi ambao wametoa mchango mkubwa mno
katika kuiboresha na kuitajirisha sanaa ya mapigano (wushu) ya China.
Fani hiyo iliasisi kwa nyakati za Ming na kustawishwa sana enzi za Qing;na
ikawa ni jambo la lazima kujifunza mbinu za kujihami ili kulinda maisha
ya jamii katika zama za udikteta umwembechai na ukandamizaji wa kitaifa.
Sanaa hiyo ilifanya kazi isiyosahaulika katika jamii hususan kuimarisha
afya, kujenga kuta imara za hulka ndani ya jamii ya Kiislamu hasa za kuvumilia
shida na kusaidiana.
Aidha, kutoogopa kufanyiwa ukatili, kuwa wakarimu na kusaidia wengine
na kutetea kwa nguvu zote haki katika jamii.
Sanaa hiyo ina taaluma nyingi, ambazo ni matokeo ya maendeleo ya mfululizo
juu ya msingi wa kupokea vilivyo bora toka kwa wengine, kufafanua na kurekebisha
kizazi kwa kizazi hata kufikia sasa.
Sanaa hiyo inatazamana na kipindi kipya cha maendeleo, imeshakuwa harakati
za kawaida za nadharia za kuimarisha afya za watu na umoja wa makabila
toka haja za kulinda kabila, dini na kujilinda katika jamii ya kimwinyi.
Sasa Wushu imeenea zaidi.
Kiuhakika sanaa hiyo ya Kiislamu inayopendwa kote duniani hata sasa,bado
haijatiliwa uzito na jamii nyingine za Kiislamu hasa za Afrika ya Mashariki
kama Tanzania, kinyume chake inawafaidisha watu wa jamii nyingine wasio
na asili nayo kuwakandamiza Waislamu!
Ukiacha wenzetu wa China wanaozifuata kwa vitendo sunna za Bwana Mtume
(s.a.w.) si kwa kumpigia dufu na kula pilau tu, Waislamu wenzetu wa Afrika
Kusini wanaikaribia Uchina katika nyanja hiyo.
Baadhi ya taasisi za Kiislamu zimelifanya somo la sanaa ya mapigano
(Martial art) kuwa ni moja ya masomo muhimu kabisa kwenye shule zao, kuanzia
madrasa za mitaani, shule za watoto wadogo hadi vyuo vya elimu ya juu.
Zipo baadhi ya madrasa zimefikia hatua ya kuwarudisha darasa (kurudia
mwaka) kwa wale wanafunzi waliofeli vibaya somo hilo. Miongoni mwa mitindo
niliyowahi kuiona ikitumiwa sana nchini humo na baadhi ya taasisi za Kiislamu
ni pamoja na Carate ya Kijapan maarufu sana kwa jina la ‘Goju lau’mtindo
ambao unafunza mbinu ngumi na staili za kujihami.
Mitindo mingine ya mapigano ni pamoja na Judo, Kungfu, Shaolin, Taiji
na Taiji Boxing, na hata shotokan na Tiechi (inner structure na outer structure).
Mitindo hiyo pamoja na Tao na Yoga wameirekebisha kidogo na kuiweka
katika sura ya Kiislamu. Hivyo kama Uchina ni mbali (ingawa mtume amesema
tutafute elimu japokuwa China)tunaweza kujifunza mengi kwa ndugu zetu karibu.
"Wapo vijana wengi wa Kiislamu Tanzania ambao ni mabingwa katika sanaa
ya mapigano, hata hivyo ustadi wao unawasaidia (unawanufaisha) madhalimu.
Ni vyema tukiitafuta njia nzuri ya kuwarejesha mastadi hawa wausadie Uislamu
na Waislamu wenzao. Itakuwa vizuri Waislamu na taasisi zao hasa misitiki
mwashule na madrasa za mitaani wakianza programu hiyo sasa".